Jumanne, 5 Mei 2015
barbra william
Hatari sana! Mkali wa Ngoma ya Chekecha Cheketua, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’ amenusurika kifo baada ya kuvamiwa nyumbani kwake na majambazi ambao walimteka mlinzi na ndugu yake mmoja kisha kuwashushia kibano kikali huku wakiwaamuru wawapeleke kwenye chumba anacholala msanii huyo,Akizungumza kwa masikitiko makubwa na mwandishi wetu Mei 2, mwaka huu, Abdul Kiba ambaye ni mdogo wa Ali Kiba, alisema usiku wa siku ya tukio alipewa taarifa na Ali Kiba kuwa amevamiwa na majambazi wenye silaha za moto hivyo alikurupuka moja kwa moja hadi Kituo cha Polisi cha Oysterbay jijini Dar ambapo waliripoti na baadaye kupata msaada wa polisi hadi eneo la tukio nyumbani kwa jamaa huyo Kunduchi Beach.
“Wakati linatokea tukio hilo nilikuwa Masaki (Dar) na jamaa yangu mmoja anaitwa Bude, kaka (Ali) alinipigia simu na kuniambia kilichotokea nasi hatukuchelewa tukaenda polisi na kuwaeleza hivyo tukaambatana nao hadi nyumbani.
“Tulikuta wamevunja mlango na kuzama ndani ambapo chumbani kwangu walichukua tivii flat screen, viatu na nguo zangu, maana kumbe wakati wanaenda chumbani kwangu walijua ni chumba cha Ali.
“Bahati nzuri majambazi walipofika walimwambia yule ndugu yetu aliyekuwa pamoja na mlinzi awaelekeze chumba cha Ali ambapo aliwapotosha kwa kuwaelekeza kwangu.
“Baada ya kuvunja mlango hawakumuona hivyo wakamuuliza akawaambia hajui labda katoka yeye akiwa amelala ndiyo wakaishia kuchukua vitu hivyo vya ndani.
“Wakati wanafanya hayo yote yeye (Ali Kiba) alikuwa akiwasikia tu chumbani kwake maana hadi wanatoka alikuwa akiwafuatilia kwa makini na hata maneno waliyokuwa wakizungumza yalikuwa yakutishia sana amani yake.
“Nashukuru kaka yangu hajaguswa, ila wameiba vitu kibao maana ukiachilia mbali tivii yangu na nguo wamechukua tivii ya sebuleni na kila kitu kilichobebeka,” alisema Abdul Kiba.
Hadi storyi hili inakwenda mitamboni, jeshi la polisi lilikuwa likiendelea na uchunguzi wa kuwasaka watuhumiwa.
Ni vyema mastaa mbalimbali ambao wanaonesha mali zao kama Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ wakaimairisha ulinzi nyumbani kwao ili kujilinda zaidi. -Mhariri
photo by:global publishers
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Search
Popular Posts
-
ALLY REHMTULAH KUJA NA UFAHARI WETU FESTIVAL Mbunifu wa mavazi nchini Tanzania Allyrehmtullah ameandaa tamasha linalokwenda kwa jina ...
-
Faida za kutumia ua la Ulimi wa Mama Mkwe kiroho ni nyingi sana, hasa kwa mtu mwenye macho ya rohoni au anayejishughulisha na mambo ya kinga...
-
UREMBO ni jambo muhimu kwa mwanamke kwa kujiweka nadhifu wakati wote ikiwa ni pamoja na kujipamba na kujifanyia usafi wa mwili. Watu wengi w...
-
JACKSON KABIRIGI'S PROFILE
-
Rangi ya mdomo ni moja ya vipodozi vinavyoongeza urembo kwa mwanamke.Kuna rangi mbalimbali za mdomo kulingana na anachopenda kupaka mrembo h...
-
Asilimia kubwa ya watu wamekuwa na tatizo la kuwa na makovu yanayosababishwa na chunusi kwa kipindi kirefu bila kupata ufumbuzi, na hii ...
-
MISS KINONDONI 2019 PRESS BONANZA Leo miss kinondoni wamefanya special bonanza kwa lengo la kuchangia kituo ch...
-
Tanzania ni moja ya nchi zilizoko chini ya jangwa la sahara afrika imekuwa na wimbi la kuongezeka kwa watu wenye ulemavu ngozi ,jamii y...
Recent Posts
Categories
Sample Text
Blog Archive
-
▼
2015
(56)
-
▼
Mei
(12)
- Kwa nini wanaume hutoa mamilioni ya manii katika k...
- Hisia nane hatari katika mapenzi
- Aina 10 ya Wanawake Wanaopendwa na Wanaume
- Hatua 5 za kuzungumza na mpenzi wako aliyekasirik...
- JINSI YA KUMTAMBUA MWANAMKE ANAYEKARIBIA KUKUACHA...
- MESEJI NZURI ZA MAPENZI KWA UMPENDAYE KWA DHATI ...
- Updated Eyebrow Tutorial
- DIY Turn Your Old Pants Into Cool Bleached, Distre...
- BEYONCE has outdone Kim Kardashian’s and Jennifer ...
- A-Z ALI KIBA ALIVYONUSURIKA KUUAWA!
- Mashabiki wa Wema Sepetu na Diamond Platnumz..Matu...
- SHETTA “NAMUOMBA MUNGU ANGEMLETA ROSE NDAUKA MAPEM...
-
▼
Mei
(12)
0 maoni:
Chapisha Maoni