Ijumaa, 21 Agosti 2015
KAA UKITAMBUA KUWA MKE NI MATUNZO, YAANI SAWA NA MGOMBA KUPALILIWA KILA WAKATI!!! Assalaam alaikum/Bwana Yesu asifiwe! Bila shaka mna afya njema wasomaji wangu. Kikubwa mjue naendelea kuwapenda, kuwathamini na kuwaheshimu kwani mmekuwa mkionesha kukubali kile ambacho nakiandika kupitia safu hii.
Ndiyo maana leo nimeamua kuwasema wanaume kwa sababu nao ni miongoni mwa watu ambao hawajakamilika na wanastahili kukumbushwa baadhi ya mambo ili ndoa zao ziwe tamu, au siyo jamani?
Ujumbe mwingi ninaopokea kutoka kwa wanaume umenifanya nigundue kuwa wengi wenu mna kasoro na mnatakiwa kuzifanyia kazi ili kulinda ndoa zenu.
Ujumbe mwingi ninaopokea kutoka kwa wanaume umenifanya nigundue kuwa wengi wenu mna kasoro na mnatakiwa kuzifanyia kazi ili kulinda ndoa zenu.
Hivi mnafahamu kitu muhimu kwa mwanamke ni suala la kuhakikisha amekula, amepata nguo nzuri na burudani faragha?
Wengi wa wanaume hawalijui hilo kabisa kwani wanadhani mwanamke akishapewa burudani ya ndoa inatosha, wanasahau kuwa kuna umuhimu wa kuhakikisha anapendeza na anakula vizuri pia.
Kuna wanaume kazi yao kuwasifia wake za watu bila kujua kuwa hata mkeo ukimjali atakuwa na mvuto na atasifiwa. Yaani mkeo tangu umemm-nunulia nguo ya harusi ndiyo imetoka, hata siku moja hujawahi kumnunulia hata leso, hujawahi kumpa ‘kijihela’ angalau akanunue nguo.
Huna mawazo ya kumpa hata pesa akanunulie ‘vijiurembo’ ili angalau akipita mbele za watu aonekane ni mke wa mtu anayethaminiwa. Hilo ni tatizo kwenu wanaume.Matunzo hamtoi inavyotakiwa, tena wengine wanajiangalia wao tu. Hivi unajisikiaje pale unapojipendezesha wewe tu wakati mkeo anaonekana yupo yupo tu? Badilikeni jamani, tena nasisitiza mbadilike!
Nimetoleo mfano mgomba kwamba unastahili kupaliliwa na kumwagilia ili uweze kukua vizuri. Vivyo hivyo kwa mkeo. Ili aonekane amependeza, hilo jukumu unalo wewe mume! Usitarajie eti kwa kuwa anajishugulisha basi ajipendezeshe mwenyewe, hiyo ni sawa kweli?
Hatukatai mke kujinunulia nguo, urembo na vitu vingine lakini je kama hana uwezo wa kufanya hivyo afanyeje? Wewe ulipoamua kumuoa si ulijiaminisha kwamba utaweza kumtunza? Sasa mbona humjali na kumtuza ipasavyo?
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Search
Popular Posts
-
Akiwa na umri wa miaka 89 aliishi katika kipindi kigumu katika miaka ya 1990 kutokana na talaka za watoto wake 3 na ukimya usiokifani...
-
ALLY REHMTULAH KUJA NA UFAHARI WETU FESTIVAL Mbunifu wa mavazi nchini Tanzania Allyrehmtullah ameandaa tamasha linalokwenda kwa jina ...
-
Msanii wa filamu nchini ambaye pia ni Miss Tanzania 2006 Wema Sepetu, kufungua duka kubwa la urembo nchini Afrika Kusini. Kwa mujibu wa c...
-
Rangi ya mdomo ni moja ya vipodozi vinavyoongeza urembo kwa mwanamke.Kuna rangi mbalimbali za mdomo kulingana na anachopenda kupaka mrembo h...
-
MISS KINONDONI 2019 PRESS BONANZA Leo miss kinondoni wamefanya special bonanza kwa lengo la kuchangia kituo ch...
-
Tamasha la kutuza watu weusi wanaon"ara kwenye fani tofauti zinazoandaliwa na televison(BET),zilifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita na...
-
Huyu ni binti mwenye umri wa miaka19 mzaliwa wa mkoa wa Morogoro amemaliza elimu yake ya msingi na sekondani mkoani morogoro. Fani ya urem...
-
barbra william Hatari sana! Mkali wa Ngoma ya Chekecha Cheketua, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’ amenusurika kifo baada ya kuvamiwa nyu...
0 maoni:
Chapisha Maoni