Alhamisi, 2 Februari 2023
On 08:27 by barbrawilliam No comments
Katika kuadhimisha miaka 46 ya chama Cha mapinduzi wanachama wa UWT Turiani wilaya ya mvomero wameshiriki upandaji wa miti karibu na mto mbulumi uliopo tarafa ya Turiani wilaya ya Mvomero ili kusaidia kuzuia madhara yanayotokana na kufurika kwa mto huo kipindi Cha mvua
Sambamba na hilo mwenyekiti wa UWT ambaye pia ni mgeni rasmi wa maadhimisho hayo ndugu Rachel Steven Kingu ameongoza ugawaji wa vifaa mbalimbali vya usafi katika zahanati ya Turiani wilaya ya Mvomero ikiwa ni kuunga mkono jitihada za serikali katika kuboresha vituo vya afya nchini.
Aidha ndugu Kingu ameshiriki zoezi la ugawaji wa kadi za Chama Cha Mapinduzi kwa wanachama wapya na kutoa hamasa kwa viongozi wa ngazi zote hasa madiwani kushirikiana na serikali katika kufanikisha adhma ya chama na serikali kwa ujumla
On 04:43 by barbrawilliam No comments
On 04:38 by barbrawilliam No comments
On 04:23 by barbrawilliam No comments
Jumatano, 1 Februari 2023
On 22:29 by barbrawilliam No comments
On 21:14 by barbrawilliam No comments
KATIBU Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kufanya uchunguzi wa bili na bei za maji kwa wananchi wilayani Malinyi mkoani Morogoro ili kupata ukweli iwapo wananchi hao wanabambikiwa bili au lah.
Kauli hiyo ameitoa leo katika Kata ya Mtimbila aliposimamishwa na wananchi akiwa katika msafara wake kuelekea Makao Makuu ya Wilaya ya Malinyi kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kama ilivyoahidiwa kwenye Ilani ya CCM.
Mara baada ya kusimamishwa eneo hilo na wananchi walitoa kero yao kuwa bili ya maji ni sambamba na gharama za kununua maji ambapo pamoja na kwamba chanzo cha maji ni cha mserereko lakini bado wanatozwa shilingi 100 kwa ndoo ya lita 20.
Aidha,wamema bei ya maji wanayotozwa kwa mwezi kwa wale ambao hawajafungiwa mita za maji za ni shilingi 7,000 na bili hiyo inalipwa kila mwezi hata kama maji hayatoki.
Akijibu kero hiyo ambayo pia imetolewa na wananchi katika Wilaya ya Kilombero,Chongolo aliagiza Takukuru kufanya uchunguzi ili kuona uhalali wa bei hizo kwani mwongozo wa malipo ya maji ya chanzo hicho ni shilingi 20, kwa ndoo moja ya maji ya lita 20.
“Takukuru,hili lichukueni lichunguzeni kuona uhalali wake,maana nimepewa kero hii mara nyingi,sasa lifanyieni kazi,”amesema Chongolo.
Chongolo yupo katika ziara ya kikazi mkoani Morogoro akiwa ameongozana na Katibu wa Halmashauri Kuuya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Sophia Mjema na Katibu wa NEC Oganaizesheni, Issa Haji(Gavu)
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)
Search
Popular Posts
-
Akiwa na umri wa miaka 89 aliishi katika kipindi kigumu katika miaka ya 1990 kutokana na talaka za watoto wake 3 na ukimya usiokifani...
-
ALLY REHMTULAH KUJA NA UFAHARI WETU FESTIVAL Mbunifu wa mavazi nchini Tanzania Allyrehmtullah ameandaa tamasha linalokwenda kwa jina ...
-
Msanii wa filamu nchini ambaye pia ni Miss Tanzania 2006 Wema Sepetu, kufungua duka kubwa la urembo nchini Afrika Kusini. Kwa mujibu wa c...
-
Rangi ya mdomo ni moja ya vipodozi vinavyoongeza urembo kwa mwanamke.Kuna rangi mbalimbali za mdomo kulingana na anachopenda kupaka mrembo h...
-
MISS KINONDONI 2019 PRESS BONANZA Leo miss kinondoni wamefanya special bonanza kwa lengo la kuchangia kituo ch...
-
Tamasha la kutuza watu weusi wanaon"ara kwenye fani tofauti zinazoandaliwa na televison(BET),zilifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita na...
-
Huyu ni binti mwenye umri wa miaka19 mzaliwa wa mkoa wa Morogoro amemaliza elimu yake ya msingi na sekondani mkoani morogoro. Fani ya urem...
-
barbra william Hatari sana! Mkali wa Ngoma ya Chekecha Cheketua, Ali Saleh Kiba ‘King Kiba’ amenusurika kifo baada ya kuvamiwa nyu...
Recent Posts
Categories
Sample Text
Blog Archive
-
▼
2023
(11)
-
▼
Februari
(7)
- UWT TULIANI WAFANYA MAAJABU KUADHIMISHA MIAKA 46 Y...
- SENETA SANGA "MLIAHIDI KUJENGA UWANJA DODOMA, UKO ...
- WAKINA BABA NAO WAKOPESHWE MBUNGE AWAKA
- Luhaga Mpina Ashangazwa na Majibu ya Waziri wa Fed...
- Waziri Mkuu Serikali Haitafumbia Macho Adhabu Shu...
- MH RAIS SAMIA AZINDUA TUME YA KUANGALIA JINSI YA ...
- CHONGOLO AIAGIZA TAKUKURU KUCHUNGUZA BILI ZA MAJI ...
-
▼
Februari
(7)