Alhamisi, 2 Februari 2023

On 08:27 by barbrawilliam   No comments
Katika kuadhimisha miaka 46 ya chama Cha mapinduzi wanachama wa UWT Turiani wilaya ya mvomero wameshiriki upandaji wa miti karibu na mto mbulumi uliopo tarafa ya Turiani wilaya ya Mvomero ili kusaidia kuzuia madhara yanayotokana na kufurika kwa mto huo kipindi Cha mvua
Sambamba na hilo mwenyekiti wa UWT ambaye pia ni mgeni rasmi wa maadhimisho hayo ndugu Rachel Steven Kingu ameongoza ugawaji wa vifaa mbalimbali vya usafi katika zahanati ya Turiani wilaya ya Mvomero ikiwa ni kuunga mkono jitihada za serikali katika kuboresha vituo vya afya nchini. Aidha ndugu Kingu ameshiriki zoezi la ugawaji wa kadi za Chama Cha Mapinduzi kwa wanachama wapya na kutoa hamasa kwa viongozi wa ngazi zote hasa madiwani kushirikiana na serikali katika kufanikisha adhma ya chama na serikali kwa ujumla
On 04:43 by barbrawilliam   No comments
On 04:42 by barbrawilliam   No comments
On 04:38 by barbrawilliam   No comments
On 04:23 by barbrawilliam   No comments

Jumatano, 1 Februari 2023

On 22:29 by barbrawilliam   No comments
On 21:14 by barbrawilliam   No comments
KATIBU Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kufanya uchunguzi wa bili na bei za maji kwa wananchi wilayani Malinyi mkoani Morogoro ili kupata ukweli iwapo wananchi hao wanabambikiwa bili au lah. Kauli hiyo ameitoa leo katika Kata ya Mtimbila aliposimamishwa na wananchi akiwa katika msafara wake kuelekea Makao Makuu ya Wilaya ya Malinyi kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kama ilivyoahidiwa kwenye Ilani ya CCM. Mara baada ya kusimamishwa eneo hilo na wananchi walitoa kero yao kuwa bili ya maji ni sambamba na gharama za kununua maji ambapo pamoja na kwamba chanzo cha maji ni cha mserereko lakini bado wanatozwa shilingi 100 kwa ndoo ya lita 20. Aidha,wamema bei ya maji wanayotozwa kwa mwezi kwa wale ambao hawajafungiwa mita za maji za ni shilingi 7,000 na bili hiyo inalipwa kila mwezi hata kama maji hayatoki. Akijibu kero hiyo ambayo pia imetolewa na wananchi katika Wilaya ya Kilombero,Chongolo aliagiza Takukuru kufanya uchunguzi ili kuona uhalali wa bei hizo kwani mwongozo wa malipo ya maji ya chanzo hicho ni shilingi 20, kwa ndoo moja ya maji ya lita 20. “Takukuru,hili lichukueni lichunguzeni kuona uhalali wake,maana nimepewa kero hii mara nyingi,sasa lifanyieni kazi,”amesema Chongolo. Chongolo yupo katika ziara ya kikazi mkoani Morogoro akiwa ameongozana na Katibu wa Halmashauri Kuuya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Sophia Mjema na Katibu wa NEC Oganaizesheni, Issa Haji(Gavu)